Marekani yapanga kupunguza safari za ndege ikiwa kufungwa kwa serikali kutaendelea

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na : Cantona Joseph|RFA

Waziri wa Uchukuzi wa Marekani
Maelezo ya picha,Waziri wa Uchukuzi wa Marekani

Waziri wa uchukuzi wa Marekani, Sean Duffy, amewaonya kuwa, kuanzia asubuhi ya Ijumaa, kutakuwa na upungufu wa asilimia 10% katika uwezo wa usafirishaji wa anga katika viwanja 40 vikuu vya ndege endapo kufungwa kwa serikali kutaendelea.

Kupunguzwa kwa safari za ndege kutakuwa kwa awamu,kuanzia 4% ya safari za ndani siku ya Ijumaa, kisha kupanda hadi 5% Jumamosi na 6% Jumapili, kabla ya kufikia 10% kamili wiki ijayo, Reuters iliripoti baada ya tangazo hilo, ikinukuu vyanzo vinne ambavyo havikutajwa.

Kufutwa kwa safari za ndege kutaathiri kati ya safari za ndege 3,500 na 4,000 kwa siku.

Uamuzi huu umetokana na ripoti zinazotolewa na wadhibiti wa trafiki ya anga, alisema Bryan Bedford, mkuu wa Utawala wa Serikali wa Anga (FAA), wakati wa mkutano na Duffy Jumatano.

“Hili ni jambo lisilo la kawaida, kama vile kufungwa kwa serikali ni jambo lisilo la kawaida, na kama vile ukweli kwamba wadhibiti wetu hawajalipwa kwa mwezi mzima ni jambo lisilo la kawaida pia,” alisema Bedford.

Wakati huu wa kufungwa kwa serikali, ambao ni mrefu zaidi katika historia ya Marekani, wadhibiti wameendelea kufanya kazi bila malipo, jambo lililosababisha baadhi yao kudai likizo za ugonjwa au kuchukua kazi za ziada.

Mara tu baada ya serikali kufungwa, viwanja vya ndege vilianza kuathirika.

Baadhi vililazimika kusimamisha ndege kwa saa kadhaa baada ya wadhibiti kudai likizo ya ugonjwa, huku wengine wakitegemea wadhibiti kutoka viwanja vingine.

Nick Daniels, rais wa chama cha wafanyakazi kinachowakilisha zaidi ya wafanyakazi 20,000 wa anga, alielezea hali hiyo kwa maneno makali: “Wadhibiti wa trafiki ya anga wanatuma ujumbe wa maandishi wakisema, ‘Sina hata pesa za kununua mafuta ya gari ili kuja kazini.’”

Duffy alionya mwanzoni mwa wiki kuwa kusitishwa kwa safari za ndege kunaweza kuanza, kwani nusu ya viwanja vikuu 30 vya ndege nchini vina uhaba wa wafanyakazi.

Aidha, aliashiria kuwa kuchukua kazi za ziada na wadhibiti wa trafiki ya anga wakati wa kufungwa kwa serikali kunaleta hatari, na aliwatishia kuwafukuza waliokosa kufika kazini.

“Wadhibiti wanapaswa kufanya uamuzi: je, ninaenda kazini bila mshahara na bila kuweka chakula mezani, au naendesha Uber, DoorDash, au kusubiri wageni mezani?” alisema Duffy katika kipindi cha ABC Jumapili.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment