Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na : Cantona Joseph|RFA

Israel imepokea mwili wa mateka wa Gaza kutoka kwa Shirika la Msalaba MwekunduPicha: Abed Rahim Khatib/Anadolu Agency/IMAGO
Israel imepokea mabaki ya mwili wa mateka mwingine wa Israel aliyekuwa akishikiliwa huko Gaza tangu shambulizi la Hamas mnamo Oktoba 7 mwaka 2023.
Israel imepokea mwili wa mateka kutoka kwa shirika la Msalaba Mwekundu huko Gaza jana Jumatano, kulingana na ofisi ya waziri mkuu, katika makabidhiano ya hivi karibuni kufanyika chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Marekani.
Ofisi ya waziri mkuu ilisema katika taarifa kwamba jeneza la mateka huyo lilikabidhiwa kwa jeshi la Israeli na idara ya ndani ya usalama, na “litapokelewa kwa sherehe ya kijeshi” kabla ya kupelekwa katika kituo cha kitaifa cha uchunguzi wa kimahabara kwa ajili ya utambuzi.
Katika taarifa ya pamoja, jeshi na shirika la upelelezi wa ndani Shin Bet baadaye walithibitisha kwamba mabaki hayo yalivuka mpaka na kuingia katika dola ya Israeli”, huku jeshi likiwahimiza umma kusubiri uthibitisho rasmi wa utambulisho wa marehemu.
Mwanzoni mwa makubaliano ya kusitisha mapigano mwezi uliopita, Hamas iliwaachilia mateka wote 20 waliosalia waliokamatwa wakati wa shambulio lake dhidi ya Israeli mnamo Oktoba 7, 2023, ambalo lilisababisha vita vya Gaza.
Kwa kubadilishana, Israeli iliwaachilia mamia ya wafungwa wa Kipalestina waliokuwa chini ya ulinzi wake.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.