Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na: Cantona Joseph|RFA

Hafla ya kuapishwa kwa Samia Suluhu Hassan imeanza katika uwanja wa kijeshi lakini raia wa kawaida hawatahudhuria.
Rais mteule wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuapishwa wakati wowote kutoka sasa baada ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa Jumatano uliokumbwa na utata.
Upinzani umeutaja uchaguzi huo kama kejeli kwa demokrasia.
Hafla hiyo inafanyika katika uwanja wa kijeshi na haitakuwa wazi kwa umma.
Picha ambazo BBC imezipata ni gwaride la jeshi tayari liko uwanjani kwa shughuli hiyo nzima ikitarajiwa kutumbuiza wageni mashuhuri watakaokuja kushuhudia uapisho wa rais mteule Samia.
TBC inapeperusha matangazo hayo mubashara kutoka Dodoma kwa taifa.
Rais Samia alitangazwa mshindi wa uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 29 kwa kujinyakulia asilimia 97.66 ya jumla ya kura zote zilizopigwa.
INEC imetangaza kwamba ushindi mkubwa wa Rais Samia ambao haujawahi kushuhudiwa nchini Tanzania katika awamu tano za kwanza za uongozi wa nchi hiyo.
Wapiga kura milioni 37 walisajiliwa kushiriki kwenye uchaguzi wa mwaka huu huku INEC ikisema kwamba Samia alipata jumla ya kura milioni 31.
Aidha tume hiyo imesema pia kwamba asilimia 87 ya waliosajiliwa kupiga kura walijitokeza kushiriki kwenye uchaguzi huo ambao ulishuhudia maandamano huku mji wa Dar es Salaam ukikabiliwa na amri ya kutotoka nja kati ya saa 12 jioni na saa 12 asubuhi.
Tayari Rais wa Zanzibar Hussein Mwinyi ameapishwa baada ya kumshinda mpinzani wake wa chama cha ACT-Wazalendo Othman Masoud.
Sherehe hiyo ya uapisho wa rais wa Zanzibar ilihudhuriwa na maafisa wakuu wa serikali, akiwemo Makamu wa Rais wa Tanzania, Philip Mpango, wanadiplomasia, na maelfu ya raia wa Zanzibar.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.