Mtandao warejea Tanzania

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na: Cantona Joseph|RFA

.

Hatimaye mtandao umerejea nchini Tanzania baada ya kufinywa kwa siku sita.

Hili limehjiri baada ya Rais Samia kuapishwa na kuchukua majukumu yake rasmi.

Katika hotuba aliyotoa wakati wa kuapishwa kwake Rais Samia alitoa maagizo kwa vyombo vya usalama kuhakikisha hali imerejea kama kawaida kwa Watanzania.

“Kamati ya kitaifa na kamata za ulinzi za mikoa na wilaya nawataka muhakikishe, kuanzia leo maisha ya wananchi yanarejea mara moja,” alisema Rais Samia.

Kuzimwa wa mtandao kulifanya mawasiliano kuwa magumu, biashara zimesimama, sekta ya utalii imedorora na hata kuwa vigumu kujua hali inavyoendelea nchini humo Tanzania.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment