Baadhi ya wasanii wafuta maudhui yanayoegemea CCM Tanzania

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na: Cantona Joseph|RFA

.

Vurugu ambazo zimeshuhudiwa nchini Tanzania zimeonekana kulenga watu mashuhuri kama vile wasanii na wanamitindo wanaodaiwa kuunga mkono serikali ba kusababisha kuvamiwa na kuharibiwa kwa biashara zao.

Kufuatia hatua hiyo, baadhi yao wamefuta picha na video walizochapisha kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na Instagram zakumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wakiongozwa na msanii wa nyimbo za bongo Naseeb Abdul almarufu Diamond Platnumz wamefuta maudhui hayo waliokuwa wakiyachapisha wakati wa kampuni za uchaguzi mkuu.

Miongoni mwa waathirika wa kwanza ni mwimbaji Shilole, ambaye mgahawa wake maarufu wa Shishi Foods, ulichomwa moto katika machafuko hayo.

Mkuu wa jeshi nchini Tanzania, Jenerali Jacob John Mkunda alitoa taarifa akilaani vurugu zinazoendelea na kusema kuwa ni ‘lazima utawala wa sheria uzingatiwe’ na kuonya kuwa wahusika watachukuliwa hatua.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment