Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na: Cantona Joseph|RFA

Wakaazi wa El-Fashir waliolazimika kuyakimbia makazi yao kutokana na mzozo unaoendeleaPicha: Muhnnad Adam/AP Photo/dpa/picture alliance
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa kukomeshwa mara moja kwa ongezeko la mapigano kati ya pande zinazohasimiana nchini Sudan.
Ameyasema hayo baada ya taarifa kuwa zaidi ya watu 460 walipigwa risasi na kuuawa katika mashambulizi yaliyofanywa na wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) katika hospitali ya wajawazito kwenye mji wa El Fashir.
Hofu yazidi kutanda baada ya RSF kudhibiti El fashir
Katika tamko lake, Guterres amesema ana wasiwasi mkubwa kutokana na ongezeko la mashambulizi ya kijeshi mjini hapo siku kadhaa baada ya wanamgambo wa RSF kutangaza kuwa wameudhibiti mji huo. Mzozo kati ya wanamgambo hao na jeshi uliibuka Sudan mwezi Aprili 2023.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.