Pakistan yaionya Afghanistan dhidi ya shambulizi lolote

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na : Cantona Joseph|RFA

Waziri wa ulinzi wa Pakistan Khawaja Mohammad Asif, ameionya Afghanistan kuwa shambulio lolote la kigaidi au la kujitoa mhanga kufa litakalofanywa na wanamgambo nchini Pakistan litasababisha jibu kali la kisasi.

Afghanistan haijatoa tamko juu ya kutibuka kwa mazungumzo kati yake na Pakistan ama pia kuhusu matamshi ya Asif, lakini shirika la utangazaji la serikali ya Afghanistan, RTA, limeripoti kuwa mazungumzo yalikwama kwa sababu ya kile ilichokiita “matakwa yasiyo na mantiki” kutoka Pakistan.

Afghanistan yasema Tehrik-e-Taliban Pakistan ni suala la ndani la Pakistan

Kulingana na RTA, Pakistan ilitaka hakikisho kwamba hakuna mashambulizi yatakayotokea kutoka Afghanistan, huku ujumbe wa Taliban ukisema kundi la Taliban la Pakistan, almaarufu Tehrik-e-Taliban Pakistan, ni suala la ndani la Pakistan.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment