Alassane Ouattara wa Ivory Coast ashinda muhula wa nne kwa kishindo

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na: Cantona Joseph|RFA

.

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara amechaguliwa kwa muhula wa nne kwa ushindi mkubwa katika uchaguzi wa marudio, kulingana na matokeo ya muda yaliyotangazwa Jumatatu, matokeo ambayo yalitarajiwa kwa kiasi kikubwa baada ya wapinzani wake wakuu kuonekana kutokuwa na ushawishi.

Alassane Ouattara mwenye umri wa miaka 83 alipata asilimia 89.77% ya kura zilizopigwa.

Mtangulizi wake, Laurent Gbagbo, alikataa kukiri kushindwa katika kinyang’anyiro hicho, na kusababisha vita vya miezi minne vilivyoua takriban watu 3,000.

Waziri wa zamani wa Biashara Jean-Louis Billon, ambaye alikubali kushindwa na Ouattara siku ya Jumapili, alipata asilimia 3.09% ya kura, huku mke wa rais wa zamani Simone Gbagbo akipata asilimia 2.42%, kulingana na matokeo yaliotolewa kwenye televisheni ya serikali na Ibrahime Coulibaly-Kuibiert, rais wa tume ya uchaguzi.

Simone Gbagbo alimpigia simu Ouattara siku ya Jumatatu kumpongeza kwa ushindi wake, chanzo kiliiambia Reuters.

Kimbunga Melissa: Jamaica inajizatiti kukabili dhoruba kali zaidi duniani ya 2025

.

Watu watatu tayari wamefariki nchini Jamaica wakati ikijiandaa na dhoruba kali zaidi duniani mwaka huu – na pengine dhoruba kali zaidi kuwahi kurekodiwa katika kisiwa hicho – huku wataalamu wa hali ya hewa wa Marekani wakionya kuhusu hali “mbaya na ya kutishia maisha”.

Na kasi ya upepo ya hadi 175mph (282km/h), Kimbunga Melissa ni dhoruba ya kitengo cha tano – nguvu ya juu zaidi. Inazidi kuongezeka na inatarajiwa kutua katika kisiwa cha Karibea mapema Jumanne.

Kimbunga hicho kimesemekana kusababisha vifo vinne nchini Haiti na Jamhuri ya Dominika, pamoja na maisha yaliyopotea huko Jamaica.

Wataalamu wanaonya kwamba mwendo wa polepole wa kimbunga Melissa unaweza kumaanisha mvua kubwa ya muda mrefu katika baadhi ya maeneo, na hivyo kuongeza hatari ya mafuriko mabaya na maporomoko ya ardhi.

Mwandishi wa habari wa Uingereza Sami Hamdi azuiliwa na mamlaka ya Marekani

.

Mwandishi wa habari wa Uingereza na mchambuzi wa vyombo vya habari Sami Hamdi, mkosoaji mkubwa wa Israeli, amekamatwa na Uhamiaji na Utekelezaji wa Forodha wa Marekani (ICE).

Akiwa katika ziara ya kuzungumza Marekani mwishoni mwa juma, Hamdi alizuiliwa na maafisa wa ICE na viza yake ikabatilishwa, msemaji wa Idara ya Usalama wa Nchi (DHS), Tricia McLaughlin, alitangaza siku ya X Jumapili.

Hamdi yuko chini ya ulinzi wa ICE akisubiri kufurushwa nchini humo, aliongeza.

Wizara ya Mambo ya Nje na DHS wanadai kuwa Hamdi anaunga mkono ugaidi na ni tishio kwa usalama wa taifa, huku kundi la utetezi wa Waislamu likisema analengwa kisiasa kinyume na haki yake ya uhuru wa kujieleza.

“Tumesema hapo awali, na tutasema tena: Merekani haina jukumu la kuwakaribisha wageni wanaounga mkono ugaidi na kudhoofisha usalama wa Wamarekani,” Wizara ya Mambo ya Nje ilisema kwenye X katika chapisho kuhusu kuzuiliwa kwa Hamdi.

Idara hiyo iliongeza kuwa itaendelea kubatilisha viza za watu wanaojihusisha na shughuli hizo.

Uchaguzi Tanzania 2025: Huduma za usafiri kusitishwa kati ya Dar es Salaam na Zanzibar siku ya uchaguzi mkuu

.

Huduma za kivuko kati ya mji wa kibiashara wa Tanzania wa Dar es Salaam na Zanzibar zitasimamishwa Oktoba 29, 2025, wakati nchi hiyo itakapokuwa na uchaguzi mkuu.

Waendeshaji pekee, Azam Marine na Zan Fast Ferries wametangaza kuwa hakuna feri zitakazoendesha shughuli zake katika mwelekeo wowote hadi Oktoba 30.

Katika taarifa tofauti, makampuni hayo mawili yamesema uamuzi wa kusimamisha huduma hizo ulifanywa ili kuwezesha ushiriki wa wapiga kura katika uchaguzi.

Vivuko vinavyoendeshwa na wawili hao, husafirisha karibu abiria 10,000 kila siku kati ya Dar es Salaam na Zanzibar.

Mabrouk Hussein, msafiri wa kawaida kati ya maeneo hayo mawili, aliiambia BBC, “Nashangaa. Kwa nini iwe hivyo? Itakuwaje ikiwa mtu anahitaji kusafiri kwa ajili ya mazishi au matibabu?

Hii si haki, inaonekana ina madhumuni ya kisiasa. Kwa nini sasa? Sio kila mtu anapenda kupiga kura.

Baadhi ya mabasi kusimamisha huduma

Baadhi ya makampuni ya mabasi ya umbali mrefu pia yametangaza kuwa huduma za kwenda na kutoka Dar es Salaam zitasitishwa.

Siku ya uchaguzi, baadhi ya mabasi hayataendesha hadi miji mikubwa kama Mwanza, Tarime, Kilimanjaro, Arusha, Tabora, Bukoba na Kigoma.

Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa) kimesema kusimamishwa kwa shughuli za usafiri kunalenga kuwawezesha wafanyakazi wa usafirishaji na abiria kupiga kura zao.

Hata hivyo, Shirika la Haki za Abiria limekosoa uamuzi huo na kudai kuwa shirika la wamiliki limeshindwa kuzingatia wajibu wa kijamii na familia.

Israel yapokea maiti ambayo Hamas inasema ni mateka aliyeachiliwa Gaza

,

Israel imepokea, kupitia Shirika la Msalaba Mwekundu, jeneza ambalo Hamas inasema lina mwili wa mateka mwingine aliyeachiliwa huko Gaza.

Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) limesema wanajeshi wake wamechukua jeneza kutoka Gaza na kurejesha mwili Israel, ambapo uchunguzi wa kitaalamu utatumika kutambua mabaki hayo.

Iwapo watathibitishwa kuwa ni wa mateka, Hamas itakuwa imewarudisha Waisraeli 16 kati ya 28 waliokufa na raia wa kigeni iliyokuwa ikiwashikilia kabla ya kuanza kwa usitishaji mapigano wiki mbili zilizopita.

Makabidhiano ya hivi punde yalikuja baada ya serikali ya Israel kusema kuwa imeruhusu mwanachama wa Hamas kuingia katika eneo ndani ya Gaza linalodhibitiwa na IDF kusaidia wafanyakazi wa Msalaba Mwekundu na wafanyakazi wa Misri kuwatafuta mateka waliobakia waliokufa.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment