RSF yashambulia mji mkuu wa Sudan kwa siku ya tatu

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na: Cantona Joseph|RFA

Wanamgambo wa RSF nchini SudanPicha: Hussein Malla/AP Photo/picture alliance

Wanamgambo wa Sudan RSF wameushambulia mji mkuu, Khartoum na uwanja wake mkuu wa ndege kwa kutumia droni.

Kwa siku ya tatu sasa, RSF imekuwa ikiulenga mji huo kwa mashambulizi.

Mashambulizi ya Alhamisi yamejiri siku moja tu baada ya ndege ya kwanza ya abiria kutua katika mji huo baada ya miaka miwili.

Maafisa wa jeshi la Sudan wamesema hayo huku afisa ambaye hakutaka kutambulishwa akisema walidungua droni hizo na hazikusababisha uharibifu.

Mashambulizi ya RSF yamefanyika wakati kundi hilo likiendeleza shinikizo dhidi ya jeshi la taifa huku mkwamo wa kupata ufumbuzi wa mzozo huo ukiendelea.

Mzozo wa Sudan ulianza mwaka 2023 kufuatia mvutano ulioibuka kati ya jeshi la taifa na kikosi cha RSF ambacho awali kilikuwa sehemu ya jeshi.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment