Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na: Cantona Joseph|RFA

Ni fursa nzuri kwa sasa upo mjini au sehemu ambayo inakua unaweza kufanikiwa haraka sana. Unakuwa unafua nguo, kupiga pasi, kurekebisha na mashine za kisasa za kufulia nguo, kama blanketi, suruali, shera,mazuria,suti nk.
ZINGATIA MAMBO HAYA ILI KUFANIKIWA KATIKA BIASHARA HII..
1. Tafuta eneo lenye msongamano wa watu au eneo ambalo lipo Karibu na makazi ya watu.Usiweke kwenye uchochoroni. Bali Karibu na ofisi, vyuo, au makazi ya watu wa kipato cha kati na juu.
2. Kuwa na mwonekano mzuri katika biashara yako
Mwonekano wa ofisi, mwonekano wa Wafanyakazi, na mpangilio mzuri kwenye biashara yako. Watu wengi wanaamini mwonekano mzuri.
3. Kuwa mwaminifu kwa wateja.
Usitoe ahadi ambayo huwezi kutimiza. Ukikuta vifaa au vitu vya thamani vya watu rudisha. Hii itakujengea jina zuri sokoni.
4. Jitangaze vya kutosha
Biashara ni matangazo, usikae kinyonge weka mabango, vipeperushi, na tumia mitandao ya kijamii kutangaza biashara yako.
5. Toa ofa na zawadi kwa wateja wako.
Wateja wengi hupendelea zawadi.. unaweza ukatoa kwa muda fulani kwa wateja wapya sabani ya kuogea au kipande cha sabuni kama zawadi au tengeneza ofa kulingana na birthday au sikukuu.
6.Wateja wako wa kuu.
Wafanyakazi wa ofisi wanaovaa suti/shati kila siku,Wanafunzi wa vyuo na shule zenye sare maalum, Wanaofanya matukio (harusi, send-off, vipindi vya TV, nk)Hoteli, migahawa, hospitali, Familia zenye kipato cha kati hadi juu
7.Vifaa na mtaji
Mashine za kufulia na kukausha nguo kubwa na ndogo, mabegi,.ndoo, maji ya kutosha.nk
Mtaji wa kuanzia TZS 5,000,000 – 10,000,000
Faida ni uhakika kuanzia Tzs 15,000 Hadi 500,000 kwa siku kama umeweka sehemu sahihi na ukapata wateja wengi.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.