Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Waziri Mkuu wa Ufaransa Sebastian Lecornu leo ameusimamisha mpango wa Rais Emmanuel Macron wa mwaka 2023 wa kuongeza muda wa kustaafu hadi miaka 64, mpaka baada ya mwaka 2027.

Waziri Mkuu wa Ufaransa Sebastien LecornuPicha: Stephane Mahe/REUTERS
Lecornu amechukua hatua hiyo kutokana na shinikizo alilowekewa na wabunge wa mrengo wa kushoto, waliokuwa wamemtaka achukue hatua hiyo ili aweze kusalimika kisiasa.
Waziri mkuu huyo anayekabiliwa na kibarua cha kunusurika kura mbili za maoni wiki hii, ametangaza hilo bungeni kama sehemu ya hatua ya mwisho ya kujaribu kuweka mazingira ya kupitisha bajeti ya mwaka 2026.
Ufaransa iko katika mgogoro mbaya zaidi wa kisiasa kuwahi kuikumba nchi hiyo katika kipindi cha miongo kadhaa huku Lecornu akiwa waziri mkuu wa sita kuteuliwa na Rais Emmanuel Macron katika kipindi cha miaka miwili.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.