Watu 42 wafariki kwenye ajali ya basi Afrika Kusini

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Ajali ya basi ilitokea Jumapili Cape Mashariki na waliokufa ni raia kutoka Zimbabwe na Malawi waliokuwa safarini kurudi katika nchi zao

Picha ya ajali ya basi iliyochapishwa na wizara ya usafiri ya Afrika KusiniPicha: Limpopo Department of Transport/Xinhua/picture alliance

Na:Cantona Joseph|RFA

Rais wa Afrika Kusini  Cyril Ramaphosa ametoa taarifa leo inayosema kwamba watu wapatao 42 wamefariki kwenye ajali ya basi iliyotokea katika eneo la milimani Kaskazini mwa nchi hiyo.

Abiria 49 wamejeruhiwa. Ajali hiyo ilitokea Jumapili mwendo wa saa kumi na mbili jioni kwenye barabara kuu ya N1 karibu na mji wa Louis Trichardt, karibu kilomita 400 kaskazini mwa mji mkuu, Pretoria.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo wengi waliofariki katika ajali hiyo kwenye mkoa wa Limpopo, ni raia kutoka Zimbabwe na Malawi waliokuwa wakielekea katika mataifa yao kutoka mji wa Gqeberha huko Cape Mashariki.

Ramaphosa amesikitishwa na ajali hiyo akisema ni huzuni kwa waafrika Kusini, Zimbabwe na Malawi kwa ujumla.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment