Shirika la INSO lakanusha madai ya upelelezi Burkina Faso

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais wa Burkina Faso Ibrahima Traore

Na:Cantona Joseph|RFA

Shirika moja lisilo la kiserikali Jumatano limekanusha madai ya mamlaka za Burkina Faso kuwa wafanyakazi wake wamehusika na upelelezi.

Haya yanafanyika siku moja baada ya utawala wa kijeshi nchinihumo kusema limewakamata wafanyakazi wake.  

Shirika la Kimataifa na Usalama, INSO, lililo na makao yake nchini Uholanzi limetoa tamko hilo kufuatia Waziri wa Usalama wa Burkina Faso, Mahamadou Sana kuwatuhumu wafanyakazi wao kwa “upelelezi na uhaini”.

Katika taarifa, shirika hilo limesema linadhamiria kufanya kila liwezalo kuhakikisha wafanyakazi wake wanaachiwa. Mkurugenzi wa shirika hilo nchini Burkina Faso ni miongoni mwa wanaoshikiliwa.

Kwa upande wake Waziri Sana amesema wafanyakazi wa shirika hilo walichukua na kusambaza kwa mataifa ya kigeni, taarifa muhimu ambazo zingetishia usalama wa Burkina Faso.

Sana ameongeza kuwa shirika hilo lilipigwa marufuku kufanya kazi nchini humo mnamo Julai 31, ila baadhi ya wafanyakazi wake waliendelea na shughuli zao kwa siri.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment