Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na:Cantona Joseph|RFA
Kundi la wanamgambo la Hamas limesema Jumatano kuwa limebadilishana na Israel orodha ya majina ya mateka na wafungwa wa Palestina watakaoachiwa, chini ya mpango wa kubadilishana wafungwa na mateka.
Wanamgambo hao vile vile wamesema wana matumaini kuhusiana na mazungumzo ya kusitisha mapigano yanayoendelea huko Misri katika mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kuvimaliza vita vya Gaza.
Kulingana na chanzo cha Kipalestina kilichoko karibu na mazungumzo, muda wa kutekelezwa kwa awamu ya kwanza ya mpango huo wa hatua 20 wa Rais Trump bado haujakubaliwa katika mazungumzo hayo yanayofanyika katika mji wa Sharm el-Sheikh.
Haya yanafanyika wakati ambapo jeshi la Israel limezuia msafarawa kundi la boti tisa unaopeleka msaada Gaza mapema leo katika Bahari ya Mediterenia.
Ripoti zinaarifu kuwa wanaharakati 145 wanaoripotiwa kuwa katika hali nzuri ya kiafya wamekamatwa na wanapelekwa katika ufukwe wa Israel kwa ajili ya kurudishwa makwao.
Haya yanafanyika baada ya wanaharakati wengine 450 akiwemo Gtreta Thunberg kuzuiwa kuingia Gaza wiki iliyopita kwa ajili ya kutoa misaada.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.