Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mfalme Charles ashitushwa na shambulizi dhidi ya sinagogi moja mjini Manchester
Na:Cantona Joseph|RFA
Mfalme Charles wa tatu wa Uingereza amesema ameshitushwa na kusikitishwa na shambulizi katika sinagogi moja mjini Machester Kaskazini Magharibi mwa Uingereza, lililowauwa watu wawili na kuwajeruhi wengine watatu.
Mfalme Charles amesema yeye na mkewe Camilla wamesikitishwa na kisa hicho kilichotokea siku muhimu kwa jamii ya kiyahudi wanapoadhimisha siku kuu ya Yom Kippur.
Mwanamume anayeaminika kutekeleza kisa hicho alilivurumisha gari nje ya sinagogi hilona kuwagonga watu waliokuwa karibu huku kukiwa pia na shambulizi la kisu. Polisi mjini humo imesema imempiga risasi na kumuua mshukiwa huyo ambae hakutajwa jina.
Akizungumza baada ya kukatiza ziara yake Copenhagen kunakofanyika mkutano wa viongozi wa Ulaya juu ya Ukraine, Waziri Mkuu wa UingerezaKier Starmer amesema polisi wamepelekwa katika masinagogi yote nchini humo kuimarisha usalama zaidi kwa mayahudi.
“Shambulio la Manchester ni la kushtua kabisa na tuko pamoja na waathirika. Niko njiani kuelekea London na nikifika nitakuwa na mkutano wa dharura. Tayari naweza kusema kuwa polisi wa ziada wamepelekwa katika masinagogi yote nchini Uingereza, na tutafanya kila tuwezalo kuilinda jamii ya kiyahudi.”
Starmer amewashukuru maafisa wa polisi kwa namna walivyolishughulikia kwa haraka tukio hilo.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.