Soko la Soka Ulaya Ijumaa: Konate atakubali kusaini mkataba mpya Liverpool?

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Ibrahima Konate
Maelezo ya picha,Ibrahima Konate

Liverpool ina mataumaini kuwa itafanikiwa kumshawishi mlinzi wa Ufaransa Ibrahima Konate, 26, kusaini kandarasi mpya huku klabu za Arsenal, Chelsea na Manchester City zikimuwania. (TBR Football)

Kiungo wa Barcelona na Uholanzi Frenkie de Jong, 28, analengwa na Manchester United. (Football Insider)

Klabu ya Bayern Munich inajiandaa kumpa kandarasi ya muda mrefu mshambuliaji wa Senegal Nicolas Jackson, 24, ambaye kwa sasa anaichezea kwa mkopo klabu hiyo ya Ujerumani kutoka Chelsea. (Bild – kwa Kijerumani – usajili unahitajika)

Manchester United imefikia mkataba na Fortaleza kumsaini kiungo wa kati wa Colombia Cristian Orozco mwenye umri wa miaka 17 mara atakapofikisha umri wa miaka 18 mwezi Julai. (Athletic)

United pia wanatazamia kukamilisha dili la mlinda lango wa Derby Muingereza Charlie Hardy, 16. (Sun)

Newcastle ni miongoni mwa vilabu vinavyofuatilia hali ya kiungo wa kati wa Ufaransa Eduardo Camavinga, 22, ambaye anafikiria kuondoka Real Madrid. (Football Insider)

Gianluigi Donnarumma
Maelezo ya picha,Kipa wa Italia Gianluigi Donnarumma

Arsenal inatarajiwa kusaini mikataba miwili na klabu ya Real Sociedad ya thamani ya pauni milioni 75 kuwasajili wachezaji wake wawili ambao ni winga wa Japan Takefusa Kubo, 24, na mlinzi wa Ufaransa Lucien Agoume, 23. (Fichajes – kwa Kihispania)

Chelsea imejiondoa katika kinyang’anyiro cha kumsajili kipa wa Italia Gianluigi Donnarumma, 26, anayeichezea Manchester kwa mkopo. (Teamtalk)

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment