Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Vikosi vya Israel vimekuwa vikiendesha operesheni zake kwenye viunga vya mji wa Gaza kwa wiki kadhaa.

Jeshi la Israeli limeanzisha mashambulizi ya ardhini leo Jumatatu ili kuuteka mji wa Gaza, Axios iliripoti, ikinukuu maafisa wa Israeli.
Jeshi la Israeli halikujibu mara moja ombi la kutoa maoni kuhusu hatua hiyo iliyoripotiwa, ambayo inakuja baada ya wiki kadhaa za mashambulizi makali ya Israel katika mji huo.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliamuru wanajeshi mwezi uliopita kuuteka mji wa Gaza, ambao anautaja kuwa ngome ya kundi la wanamgambo wa Hamas ambalo lilianzisha shambulizi ya ghafla Oktoba 2023 dhidi ya Israel.
Jeshi tangu wakati huo limeuzingira Ukanda wa Gaza, na kusababisha janga la kibinadamu na uharibifu mkubwa, uhamishaji wa watu wengi na uhaba mkubwa wa chakula na maji.
Vikosi vya Israel vimekuwa vikiendesha operesheni zake kwenye viunga vya mji wa Gaza kwa wiki kadhaa, vikikaribia katikati mwa mji huo ambapo takriban Wapalestina milioni 1 walikuwa wametafuta hifadhi mwezi uliopita.
“Gaza inaungua,” Waziri wa Ulinzi wa Israeli Israel Katz alisema katika ujumbe kwenye mtandao wa X mapema Jumanne. “IDF inashambulia kwa nguvu kwenye miundombinu ya kigaidi na wanajeshi wa IDF wanapigana kwa ujasiri ili kutengeneza mazingira ya kuachiliwa kwa mateka na kushindwa kwa Hamas.”
Mazoezi ya kijeshi ya Belarusi na Urusi yanaonekana kutoa ujumbe kwa Ulaya

Vikosi vya kijeshi vya Belarusi na Urusi vinashiriki katika mazoezi ya pamoja kwenye uwanja wa Borisovsky, tukio ambalo linashuhudiwa na vyombo habari vya kimataifa.
Katika uwanja mkubwa wa maili 45 (72km) kutoka mji mkuu wa Belarus Minsk, vita vinaendelea.
Kuna milipuko mikubwa huku washambuliaji wa Sukhoi-34 wakidondosha mabomu. Moshi mwingi unafanya anga kuwa giza.
Eneo lote linatoa mwangwi na makombora ya mizinga yanayolipuka. Helikopta ya kijeshi ya kivita inajiunga na shambulio hilo, huku ndege zisizo na rubani zikitanda angani kutazama uharibifu.
Haya yote ni mazoezi tu. Ni sehemu ya mazoezi ya kijeshi ya Zapad-2025 (“West 2025”). Maafisa wengine wa kijeshi kutoka balozi mbalimbali pia walikuwepo kushuhudia kinachoendelea.
Haya ni mazoezi yaliyopangwa ya “West 2025” ambayo hufanyika kila baada ya miaka minne.
Moscow na Minsk zinashikilia kuwa mazoezi hayo ni ya kujilinda tu, kwamba yameandaliwa ili kuimarisha usalama wa Urusi na Belarusi na kukabiliana na tishio lolote la nje linaloweza kutokea.
Madai kama hayo yalisikika miaka mitatu na nusu iliyopita.
Mnamo Februari 2022 BBC ilitembelea Belarusi ili kuripoti juu ya mazoezi ya kijeshi ya Belarusi-Urusi.
Zoezi hilo lilipokamilika, badala ya kurejea nyumbani wanajeshi wa Urusi walivamia nchi jirani ya Ukraine kutoka eneo la Belarus.
Wakati huu Belarus inasisitiza kuwa haina chochote cha kujificha.
Mshukiwa wa Charlie Kirk ahusishwa na eneo la uhalifu kwa DNA, asema mkuu wa FBI

DNA kwenye taulo iliyozungushiwa bunduki inayoshukiwa kutumika kumuua Charlie Kirk imelingana na DNA ya mshukiwa aliye kizuizini, mkurugenzi wa FBI amesema siku ya Jumatatu.
Tyler Robinson, 22, alikamatwa kufuatia kifo cha Kirk katika hafla kwenye Chuo Kikuu cha Utah Valley mnamo Jumatano. Bunduki aina ya ‘bolt-action’ ilipatikana karibu na eneo la tukio huku bisibisi ikionekana kwenye paa ambapo risasi iliyomuua mfuasi huyo ilifyatuliwa.
“Naweza kusema leo kwamba DNA iliyokuwa kwenye taulo iliyofungwa kwenye bunduki na DNA kwenye bisibisi zimelingana na ile ya mshukiwa aliye kizuizini,” Kash Patel aliiambia Fox and Friends.
Mashtaka rasmi yanatarajiwa wiki hii.
Mkurugenzi wa FBI – ambaye anatarajiwa kuhojiwa katika kikao cha Bunge siku ya Jumanne – pia alitaja barua iliyogunduliwa nyumbani kwa mshukiwa, ambayo iliapa “kumuondoa” Kirk.
“Kimsingi inasema… ‘Nina fursa ya kumuondoa Charlie Kirk’, na nitatumia fursa hiyo. Maelezo hayo yaliandikwa kabla ya Kirk kupigwa risasi,” alisema Patel.
Aliongeza, “ingawa imeharibiwa, tumepata ushahidi wa kitaalamu wa barua hiyo”.
Vijana wa China kulipa $300,000 kwa kukojoa kwenye supu

Vijana wawili ambao walikojoa kwenye sufuria ya mchuzi kwenye mkahawa mmoja wameagizwa kulipa Yuan 2.2m ($309,000; £227,000) kwa kampuni mbili za upishi nchini Uchina.
Tukio hilo, lililotokea Februari katika tawi la Shanghai la kampuni kubwa ya Uchina ya Haidilao na lilisababisha ukosoaji mkubwa baada ya vijana hao wa miaka 17 kuchapisha video ya kitendo chao mtandaoni.
Hakuna kilichoonyesha kwamba kuna mtu yeyote aliyekunywa supu hiyo iliyokojolewa lakini mgahawa wa Haidilao ulikuwa amejitolea kulipa maelfu ya waliokula katika mkahawa huo siku zilizofuata.
Mnamo mwezi Machi, Haidilao ilisema imeingia hasara ya zaidi ya Yuan 23m, kama kiasi ambacho kilifidia wateja juu ya tukio hilo.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.