Bunge lapinga maazimio ya EU kuhusu kuachiwa kwa Victoire Ingabire

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Wabunge wa Rwanda, Jumatatu ya wiki hii walipitisha azimio kulaani wito wa hivi karibuni wa bunge la umoja wa Ulaya lililoitaka serikali ya Kigali, kumuachia huru bila masharti, mwanasiasa Victoire Ingabire.

Mwanasiasa wa upinzani nchini Rwanda Victoire Ingabire.
Mwanasiasa wa upinzani nchini Rwanda Victoire Ingabire. AP – Shant Fabricatorian

Kulingana na wabunge hao, hatua ya Umoja wa Ulaya inaiingilia mfumo wa mahakama wa Rwanda pamoja na kukiuka uhuru wa taifa hilo la Afrika Mashariki.

Ingabire alikamatwa mwezi Juni mwaka huu akituhumiwa kutegeneza kikosi cha kigaidi kwa malengo ya kuchochea vurugu.

Mahakama imetupilia mbali rufaa  ya Victoire Ingabire ya kupinga kuendelea kuzuiliwa.
Mahakama imetupilia mbali rufaa ya Victoire Ingabire ya kupinga kuendelea kuzuiliwa. ASSOCIATED PRESS – Shant Fabricatorian

Kufuatia tuhuma hizo, Umoja wa Ulaya katika maazio yake ya tarehe 11 ya mwezi huu, ulisema mashtaka dhidi ya mwanasiasa huyo yamechochewa kwa misingi ya kisiasa, ukiitaka Rwanda kuyaondoa mara moja.

Hii si mara ya kwanza kwa Ingabire kushtakiwa na Kigali ambapo mwaka wa 2013 alifungwa jela miaka 15 kwa makosa ya kuchochea uasi kabla ya kuachiwa mwaka wa 2018 kwa msamaha wa Rais.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment