Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Urusi imefanya mashambulizi makubwa usiku kucha katika maeneo ya kusini na katikati mwa Ukraine, mamlaka imesema, huku Ukraine ikivishambulia vinu vya kusafisha mafuta vya Urusi.
Urusi yafanya mashambulizi makubwa dhidi ya Ukraine, huku Kyiv ikipiga vinu vya kusafisha mafuta

Urusi imefanya mashambulizi makubwa usiku kucha katika maeneo ya kusini na katikati mwa Ukraine, mamlaka imesema, huku Ukraine ikivishambulia vinu vya kusafisha mafuta vya Urusi.
Mwanamke mmoja aliuawa katika eneo la kusini mwa Zaporizhzhia na watu 30 walijeruhiwa – ikiwa ni pamoja na watoto watatu – kulingana na maafisa wa eneo hilo.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alisema Moscow ilirusha zaidi ya ndege 500 zisizo na rubani na makombora 45, na kushambulia mikoa 14 kote nchini.
Kufuatia shambulio hilo, wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema “maeneo yote yaliyolengwa na shambulio hilo yamefikiwa”
Haya yanajiri huku kukiwa na juhudi zinazoendelea za kimataifa za kupata makubaliano ya amani kati ya mataifa hayo mawili yanayopigana – na siku chache baada ya Ukraine kukabiliwa na shambulio la pili kubwa la angani hadi sasa, huku watu 23 wakiripotiwa kuuawa siku ya Alhamisi.

Huko Dnipropetrovsk, Gavana Serhiy Lysak alisema eneo hilo “linakabiliwa na shambulio kubwa” mara moja huku akiwaonya watu wajijifiche.
Ni usiku wa pili mfululizo Dnipropetrovsk inalengwa. Mapema wiki hii, Kyiv alikiri kwamba jeshi la Urusi lilikuwa limeingia katika eneo hilo na linajaribu kuweka msingi.
Ufaransa yakosoa kufutwa kwa viza ya Mahmoud Abbas ya kuhudhuria mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa

Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Noël Barrow ameikosoa Washington kwa kuwanyima viza maafisa wa Palestina kabla ya Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwezi ujao. Ameuambia mkutano wa Umoja wa Ulaya kwamba kusiwe na vikwazo vya kufikia Umoja wa Mataifa.
Ufaransa ni miongoni mwa nchi kadhaa zinazopanga kulitambua taifa la Palestina katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka huu.
Marekani inasema haitatoa viza kwa maafisa wa Palestina kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa utakaofanyika mwezi ujao mjini New York.
Kwa hiyo, wizara ya .ambo ya nje ya Marekani ilitangaza kwamba viza ya Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mahmoud Abbas ya kuhudhuria Umoja wa Mataifa “imefutwa” na hatoweza kuhudhuria mkutano huo.
Ofisi ya Mahmoud Abbas iliutaja uamuzi wa Marekani wa kubatilisha viza kuwa ni wa kushangaza na kusema kuwa hatua hiyo “inapingana kabisa na sheria za kimataifa na makubaliano ya Umoja wa Mataifa, hasa ikizingatiwa kuwa taifa la Palestina ni mwanachama waangalizi wa Umoja wa Mataifa.”
Takriban watu 70 wafamaji katika ajali ya boti ya wahamiaji kutoka Afrika Magharibi, Gambia yasema

Takriban watu 70 wamekufa maji wakati mashua iliyokuwa imebeba wahamiaji ilipopinduka katika pwani ya Afrika Magharibi, wizara ya mambo ya nje ya Gambia ilisema Ijumaa jioni, katika mojawapo ya ajali mbaya zaidi katika miaka ya hivi karibuni katika njia maarufu ya uhamiaji kuelekea Ulaya.
Watu wengine 30 wanahofiwa kufariki baada ya boti , inayoaminika kuondoka kutoka Gambia na kuwabeba raia wengi wa Gambia na Senegal, kuzama katika pwani ya Mauritania mapema Jumatano, wizara ilisema katika taarifa yake.
Ilikuwa imebeba takriban abiria 150, 16 kati yao walikuwa wameokolewa. Mamlaka ya Mauritania ilipata miili 70 siku ya Jumatano na Alhamisi, na maelezo ya mashahidi yanaonyesha zaidi ya 100 wanaweza kuwa wamekufa, taarifa hiyo ilisema.
Njia ya uhamiaji ya Atlantiki kutoka pwani ya Afrika Magharibi hadi Visiwa vya Kanari, ambayo hutumiwa na wahamiaji wa Kiafrika wanaojaribu kufika Uhispania, ni moja ya njia mbaya zaidi ulimwenguni.
Zaidi ya wahamiaji 46,000 haramu walifika Visiwa vya Canary mwaka jana, kulingana na Umoja wa Ulaya.
Zaidi ya 10,000 walikufa wakijaribu safari, ongezeko la 58% zaidi ya 2023, kulingana na kikundi cha haki cha Caminando Fronteras.
Spika wa zamani wa bunge la Ukraine Parubiy apigwa risasi na kuuawa huko Lviv

Spika wa zamani wa bunge la Ukraine Andriy Parubiy ameawa kwa kupigwa risasi katika mji wa magharibi wa Lviv siku ya Jumamosi na msako unaendelea kumtafuta muuaji huyo, Taarifa ya Reuters imesema.
Ofisi ya Mwendesha mashtaka mkuu imesema kuwa mtu mwenye silaha alimfyatulia risasi kadhaa Parubiy na kumuua papo hapo. Mshambuliaji huyo alikimbia na msako ulianzishwa, ilisema.
Parubiy, 54, alikuwa mbunge, na akawa spika wa bunge kutoka Aprili 2016 hadi Agosti 2019, na alikuwa mmoja wa viongozi wa maandamano mnamo mwaka 2013-14 akitaka uhusiano wa karibu na Umoja wa Ulaya.
Pia alikuwa katibu wa Baraza la usalama na ulinzi la kitaifa la Ukraine kuanzia Februari hadi Agosti 2014, kipindi ambacho mapigano yalianza mashariki mwa Ukraine na Urusi kutwaa rasi ya Crimea.
Maafisa hawakutoa dalili ya haraka kama mauaji hayo yana uhusiano wa moja kwa moja na vita vya Urusi nchini Ukraine .
“Waziri wa Mambo ya Ndani Ihor Klymenko na Mwendesha mashtaka mkuu Ruslan Kravchenko wameripoti hivi punde kuhusu hali ya kwanza inayojulikana ya mauaji ya kutisha huko Lviv. Andriy Parubiy ameuawa,” Rais Volodymyr Zelenskiy aliandika kwenye X.
Alituma rambirambi zake kwa familia ya Parubiy na wapendwa wake, na kuongeza: “Vikosi vyote muhimu na njia zote zinahusika katika uchunguzi na kumtafuta muuaji.”
Hamas: Mpango wa Israel wa kuuteka mji wa Gaza unayaweka maisha ya mateka hatarini

Hamas imeonya kuwa iwapo jeshi la Israel litatekeleza mpango wake wa kuuteka mji wa Gaza, maisha ya kila mateka huko yatakuwa hatarini.
Hamas pia ilisema kuwa mateka katika mji wa Gaza “wako katika kiwango sawa cha hatari kama jeshi la Israel huko.”
Kundi hilo pia lilisema litajaribu kuwalinda mateka waliosalia “kwa kadiri inavyowezekana.”
Hamas ilitoa onyo hilo baada ya jeshi la Israel kutangaza Gaza kuwa “eneo la vita.”
Mmoja wao, Alan Weiss mwenye umri wa miaka 56, anaaminika kuuawa katika mashambulizi ya Oktoba 7, na wa pili bado hajatambuliwa.
Jeshi la Israel limesema lilipata mwili wa Ilan Weiss wakati wa operesheni huko Gaza.
Aliuawa katika shambulio la Hamas kusini mwa Israel mnamo Oktoba 7, 2023.
Shambulio hilo liliua watu 1,200 na Hamas walichukua mateka 251. Kisha Israel ilianzisha vita vya kila namna dhidi ya Hamas katika Ukanda wa Gaza ambayo inaendelea hadi leo.
Kulingana na takwimu za mamlaka ya afya katika eneo hilo, zaidi ya Wapalestina 63,000 wameuawa katika mzozo huo tangu wakati huo.
Ilan Weiss aliuawa katika shambulio la Hamas tarehe 7 Oktoba katika makazi ya Wayahudi ya Kibbutz Be’er Sheva, na mwili wake ukahamishiwa Gaza.
Wanaharakati wa Ghuba wapanga kusafiri kwa meli hadi Gaza ili kuvunja kizuizi

Wakati mwezi Agosti unamalizoka, wanaharakati wa Ghuba wanajiandaa kuzindua Meli ya Ghuba inayoitwa ”Global Resilience Flee” chini ya kauli mbiu: “Wananchi wa Ghuba wanasafiri kuvunja mzingiro.”
Hii ni sehemu ya kile wanachoeleza kuwa ni vuguvugu kubwa zaidi na lisilo na kifani la mashirika ya kiraia duniani, “Muungano wa kimataifa wa kuvunja mzingiro wa Gaza.”
Harakati hii ni sehemu ya “Global Resilience Fleet,” ambayo inajumuisha wanaharakati kutoka nchi 44 duniani kote.
Vuguvugu hili linajumuisha kwa pamoja pamoja mipango kama vile Maghreb Steadfastness Flotilla, Muungano wa Kimataifa wa Flotilla wa Uhuru, Harakati za Ulimwenguni kuhusu Gaza, na Uthabiti wa vuguvugu la Nusantara.
Wanaharakati hawa wanaamini kwamba hatua za kiraia na maarufu zimekuwa jambo la lazima mbele ya kile wanachokiona kuwa kimya rasmi na kutochukuliwa hatua za kimataifa.
Msafara wa kwanza wa muungano huo umepangwa kuondoka kutoka bandari za Uhispania mnamo Agosti 31, ukifuatiwa na msafara wa pili kutoka Tunisia mnamo Septemba 4, na meli zingine zitajiunga kutoka bandari za Mediterania baadaye.
Juhudi hizi zote zinalenga kuvunja kizuizi cha majini kilichowekwa kwenye Ukanda wa Gaza, ambacho wanaamini kuwa kinasababisha maafa ya kibinadamu.
Wengi kusoma mwisho
Haya yanajiri baada ya kile kinachojulikana kama “Maandamano ya Kimataifa hadi Gaza” kushindwa kufika Ukanda wa Gaza kwa njia ya ardhi kupitia Misri mwezi Juni mwaka jana, licha ya ushiriki wa mamia ya watu kutoka nchi 80.
‘Nywele zako halisi ni zipi?’ Wigi na kucha za Cardi B viliwashangaza mawakili

Cardi B amekuwa akifuatiliwa kwa karibu wiki hii mahakamani baada ya kufika katika eneo la mashahidi mjini Los Angeles kuiambia mahakama kuwa hakumshambulia mlinzi anayemshtaki kwa kosa la kumshambulia.
Rapa huyo wa Marekani anadaiwa kumkwaruza shavu Emani Ellis kwa kucha ya inchi 3 (7.5cm) na kumtemea mate wakati wa ugomvi nje ya ofisi ya daktari mnamo 2018, na kumuacha mlinzi huyo “akiwa na kiwewe”.
Cardi alieleza kuwa Bi Ellis alivamia faragha yake kwa kurekodi filamu na kumfuata kinyume na mapenzi yake na kumwambia mtu kwa simu kuhusu kupata ujauzito ambao haukujulikana kwa umma. Kulikuwa na “mashambulizi ya maneno”, nyota huyo alisema – lakini alisisitiza “haikuwa ya kimwili”.
Wakati wa ushahidi, matukio mbalimbali za kesi ya madai yalienea, kama vile baadhi ya maoni ya Cardi B, sura yake namuonekano wake wakati wa kesi.
Cardi B aligeuza mitindo mbalimbali ya nywele kwa ajili ya kuhudhuria mahakamani wiki hii, ikiwa ni pamoja na wigi nyeusi iliyokatwa.
Katika tukio moja lilioshirikishwa sana na watumiajia wa mtandao , wakili alimuuliza Cardi B kuhusu nywele zake.
“Jana ulikuwa na nywele nyeusi, nywele fupi. Leo ni wigi ya rangi ya manjano na ndefu. Je, nywele zako ni zipi halisi? Au zote mbili ni halisi?”
“Haya ni mawigi,” Cardi B alijibu kwa kicheko na sura ya kuchekesha.
“Sawa. Samahani, sikujua hilo. Ni wigi nzuri leo, basi,” wakili alijibu.
Kisha akasogea kwenye kucha za Cardi B, akimuuliza ni za muda gani.
“Kadiria tu, kadirio lako litakuwa bora tu, sitaki uchukue rula kuzipima,” alisema.
“Lazima iwe chini ya inchi moja,” alijibu.
Kesi hiyo inatarajiwa kukamilika wiki ijayo. Huu hapa ni muhtasari wa kile ambacho kimetokea hadi sasa.
Mahakama ya Marekani yasema ushuru mwingi aliouweka Trump kwa mataifa ni kinyume cha sheria

Mahakama ya rufaa nchini Marekani imeamua kuwa ushuru mwingi uliotolewa na Rais wa Marekani Donald Trump ni kinyume cha sheria, hivyo basi kutayarisha mpambano wa kisheria ambao unaweza kuathiri ajenda yake ya sera za kigeni.
Uamuzi huo unaathiri ushuru wa Trump, uliowekwa kwa nchi nyingi ulimwenguni, pamoja na ushuru mwingine uliowekwa kwa nchi za China, Mexico na Canada.
Katika uamuzi wa Mahakama ya Rufaa ya Marekani ya shirikisho ilikataa hoja ya Trump kwamba ushuru huo unaruhusiwa chini ya sheria ya dharura ya nguvu za kiuchumi, ikiziita “batili na kinyume cha sheria”.
Uamuzi huo hautaanza kutekelezwa hadi tarehe 14 Oktoba ili kuwapa muda watawala kuitaka Mahakama ya Juu zaidi kushughulikia kesi hiyo.
Trump aliikosoa mahakama ya rufaa na uamuzi wake akisema: “Ikiwa itaruhusiwa kusimamishwa, uamuzi huu utaangamiza Marekani kihalisi.”
“Leo Mahakama ya Rufaa ya Wanachama wa Juu ilisema kimakosa kwamba ushuru wetu unapaswa kuondolewa, lakini wanajua Marekani itashinda mwishowe,” aliandika.
“Kama ushuru huu utasitishwa, litakuwa janga kubwa kwa nchi. Itatufanya kuwa dhaifu kifedha, na inabidi tuwe na nguvu.”
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.