Njia Nne Ambazo Mungu Huwa Anazitumia Kumuinua Mkombozi Wa Familia…

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

i. Kupitia ELIMU au UJUZI
ii. Kupitia BIASHARA
iii. Kupitia CHEO/NAFASI
iv. Kupitia KIPAJI

Katika Makala Hii Tutazungumzia Njia Ya Pili

– kupitia Biashara

Kwenye eneo hili, ni pale mtu anapoinuliwa na kupewa kibali cha kipekee na Mungu kufanikiwa katika biashara.

Mtu wa namna hii, mara nyingi huwa anaanzia chini wakati kila mtu anamuona na kisha anakuwa mkubwa kwenye eneo lake la biashara kiwango cha kuwa ni tegemeo la kifedha katika ukoo au familia yake.

Mara nyingi watu wa namna hii, huwa wanakuwa wameonekana na kila mtu tangu wakiwa wanaanza hadi wanapokuwa wakubwa kabisa na wakiwa tegemeo la kutosha kwenye familia zao.

Hii inaweza kutokea kwa sababu katika familia husika, hakuna mtu ambaye amefanikiwa kuinuka kielimu/ujuzi na badala yake, Mungu anaamua kutumia njia hii ili kuwakwamua familia husika kutoka kwenye changamoto zao.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment