Newcastle bado hawajapokea ofa ya Isak – Howe

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Newcastle bado hawajapokea ofa ya kumnunua mfungaji bora wao Alexander Isak, amesema meneja Eddie Howe.

Mshambuliaji huyo wa Uswidi anafuatilia machaguo alionayo kwa ajili ya uhamisho wa majira ya kiangazi na hajasafiri katika ziara ya kujiandaa na msimu mpya wa timu hiyo barani Asia, ingawa mwanzoni Newcastle walisema ana “jeraha dogo la paja”.

Chanzo kimoja kimeiambia BBC Sport kwamba Liverpool bado wanamtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, licha ya kumsajili Hugo Ekitike kwa dau la awali la £69m.

Magpies walikuwa wameshikilia kuwa Isak hauzwi na ingawa Howe anakiri kuwa “hayuko katika udhibiti kamili” wa mustakabali wa mchezaji huyo, anasema bado hakuna ofa iliyowasilishwa.

“Bado ni mchezaji wetu. Ana mkataba na sisi,” Howe alisema katika mkutano na wanahabari mjini Seoul.

“Sisi, kwa kiwango fulani, tunadhibiti kile kinachofuata kwake. Ninaamini kuwa bado uwezekano huo upo.”

“Matamanio yangu ni kwamba abaki, lakini hilo haliko katika udhibiti wangu kikamilifu. Hatujapokea ofa rasmi kwa Alex, kutoka kwa klabu yoyote.”

Isak alijiunga na Newcastle kutoka Real Sociedad mwaka 2022 kwa mkataba wa thamani ya £60m na bado ana miaka mitatu kwenye mkataba wake.

Amefunga mabao 62 katika mechi 109 akiwa na Magpies, yakiwemo 27 katika mashindano yote msimu uliopita.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment