Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Kiongoziwa Iran Ayatollah Khamenei amesema kwamba kile Marekani na nchi za Magharibi “zinawasilisha kama nyuklia, urutubishaji wa madini ya urani na ukandamizaji wa haki za binadamu ni visingizio” na kwamba tatizo lao kuu ni “elimu na umoja wa Wairani.”
Akitoa hotuba ya dakika nane katika makaazi yake, Khamenei alisema Iran “haitaachana na maarifa ya wigo mpana.”
Ayatollah Khamenei amehudhuria kumbukumbu ya siku ya 40 ya vifo vya watu waliouawa katika vita vya siku 12 na Israel na kuziambia familia zao: “Upinzani wao ni kwa mwamko mpya na uwezo wa nchi ya Jamhuri ya Kiislamu katika nyanja mbalimbali za kisayansi, kibinadamu, kiufundi na kidini
Wakati wa vita na Israel na kwa siku 22 baadaye, Ayatollah Khamenei hakuonekana kwenye hafla zozote za hadhara hadi alipojitokeza kwa mara ya kwanza tarehe 5 Julai 2025, katika sherehe za kuadhimisha mwezi wa Muharram.”
Katika hotuba yake ya hivi karibuni, Bwana Khamenei alihutubia familia za watu waliouawa katika vita na Israel na kusema: “Kupanuka kwa elimu mbalimbali hakutatupiliwa mbali, na kupitia upofu wa adui, tutaweza kuifikisha Iran kwenye kilele cha maendeleo na utukufu.”
Matamshi ya Ayatollah Khamenei yanashuhudiwa siku moja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump, akiwa pamoja na Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer huko Scotland Jumatatu, Julai 28, kuonya kwa mara nyingine tena kwamba Marekani itashambulia tena ikiwa Iran itajenga upya “uwezo wake wa nyuklia.”
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.