Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

UNAIDS itatoa ripoti yake ya kwanza juu ya maambukizo ya VVU duniani tangu Marekani kupunguza mgao wake baadaye hii leo huko Johannesburg.
UNAIDS, Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na UKIMWI linakadiria kwamba huenda kukawa na maambukizi mapya ya VVU milioni sita, na vifo milioni nne vinavyohusiana na UKIMWI, kufikia mwaka 2029, kufuatia kupunguzwa kwa fedha za misaada ya kibinadamu na Marekani.
Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI ulimwenguni.
Pia ilikuwa ni mpokeaji mkubwa wa fedha za UKIMWI kutoka Marekani hadi Machi mwaka huu, wakati utawala wa Rais Trump ulitangaza kufungwa kwa shirika la USAID.
Pesa hii ilisaidia nchi kupunguza kiwango chake cha maambukizo mapya ya VVU kwa zaidi ya 60% tangu kilele chake mnamo 2000.
Pia ilifanya nchi hiyo kuwa moja ya waongozaji katika utafiti wa VVU ulimwenguni.
Mwezi uliopita vyuo vikuu vya juu vya Afrika Kusini viliomba serikali madola ya mamilioni, ili kuendelea na utafiti huu, ambao baadhi umesitishwa kwa sababu ya kupunguzwa kwa fedha na Marekani.
Siku ya Jumatano tarehe 9/07/2025, serikali ya Afrika Kusini na wafadhili wa kimataifa waliahidi karibu dola milioni 54 ili kukabili palipo na mapungufu.
Lakini ikizingatiwa kuwa mwaka jana Marekani ilitumia mara nane ya kiwango hicho kwa ufadhili wa VVU Afrika Kusini, kiwango hiki hakitatosha kutimiza hitaji lililopo.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.