Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Utawala wa Trump unamwekea vikwazo mjumbe maalum wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa Francesca Albanese, mkosoaji mkubwa wa mashambulizi ya kijeshi ya Israel huko Gaza.
Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio alihusisha hatua hiyo na uungaji mkono wake kwa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), ambayo baadhi ya majaji wake tayari wamewekewa vikwazo na Marekani.
Rubio alisema Marekani inamuwekea vikwazo Albanese kwa kushirikiana moja kwa moja na ICC katika juhudi zake za kuwafungulia mashitaka raia wa Marekani au Israel, ikimtuhumu kuwa hafai kuhudumu kama mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa.
Vikwazo hivyo huenda vikamzuia Albanese kusafiri kwenda Marekani na vitazuia mali yoyote aliyo nayo nchini humo.
Hii ni hatua ya hivi karibuni zaidi ya utawala wa Trump unapoendesha kampeni dhidi ya ICC, ikiwa tayari imewawekea vikwazo majaji wake wanne.
Marekani ilichukua hatua hiyo baada ya mahakama ya ICC mwaka jana kutoa kibali cha kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na aliyekuwa Waziri wake wa Ulinzi wakati huo Yoav Gallant kwa tuhuma za uhalifu wa kivita huko Gaza, tuhuma wanazokanusha.
Hatua hiyo huenda ikazua msukosuko kutoka kwa wale wanaotaka uwajibikaji kuhusu idadi ya vifo vya raia kutokana na mashambulizi ya kijeshi ya Israel huko Gaza.
Jeshi la Israel lilianzisha kampeni huko Gaza kujibu shambulio lililoongozwa na Hamas kusini mwa Israel tarehe 7 Oktoba 2023, ambapo takriban watu 1,200 waliuawa na wengine 251 walichukuliwa mateka.
Takriban watu 57,575 wameuawa huko Gaza tangu wakati huo, kulingana na wizara ya afya ya eneo hilo inayoendeshwa na Hamas.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.