Trump na Netanyahu wakutana kwa mara ya pili kuzungumzia usitishaji wa mapigano Gaza

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Rais wa Marekani Donald Trump na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wamekutana kwa mara ya pili mjini Washington kujadili juhudi za kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano ukanda wa Gaza.

Mkutano huo unafanyika baada ya mjumbe wa Trump Mashariki ya Kati Steve Witkoff kusema Israel na Hamas walikuwa na suala moja ambalo bado hawajakubaliana katika mpango wa kusitisha mapigano wa siku 60.

Netanyahu alifika Ikulu ya Marekani muda mfupi baada ya 17:00 EST (21:00 GMT) Jumanne kwa mkutano huo, ambao haukuwa wazi kwa waandishi wa habari.

Mkutano wa viongozi hao wawili ulidumu karibu masaa mawili.

Kabla ya majadiliano kuanza tena Jumanne, chanzo cha Wapalestina kinachofahamu mazungumzo hayo kiliiambia BBC kuwa hawajapiga hatua yoyote.

Duru ya hivi punde ya mazungumzo kati ya Hamas na Israel ilianza Jumapili.

Vita vinavyoendelea Gaza vilianza tarehe 7 Oktoba 2023 wakati Hamas iliposhambulia Israel, na kuua watu 1,200 na kuchukua mateka 251, kulingana na takwimu za Israel.

Mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Israel yameua takriban 57,500 huko Gaza kulingana na wizara ya afya ya eneo hilo inayoendeshwa na Hamas.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment