Instagram yashutumu kimakosa baadhi ya watumiaji ikidai wamekiuka sheria za unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Watumiaji wa Instagram wameiambia BBC kuhusu “mfadhaiko mkubwa” juu ya kufungiwa akaunti zao baada ya kushutumiwa kimakosa na jukwaa hilo kwa kukiuka sheria zake za unyanyasaji wa kingono kwa watoto.

BBC imewasiliana na watu watatu ambao waliambiwa na kampuni yao kubwa ya Meta kwamba akaunti zao zilikuwa zimefungwa kabisa, lakini wakazirejesha muda mfupi baadaye, baada ya kuangaziwa na waandishi wa habari.

“Nimepoteza usingizi kwa saa kadhaa, nikijihisi kutengwa. Haikuwa hali rahisi, bila kusahau mashtaka kama hayo dhidi yangu,” mmoja wa wanaume aliambia BBC News.

Meta ilikataa kutoa maoni.

BBC News imewasiliana na zaidi ya watu 100 wanaodai kupigwa marufuku kimakosa na Meta.

Baadhi wanazungumzia kuhusu upotevu wa mapato baada ya kufungiwa akaunti zao za kibiashara, huku wengine wakiangazia uchungu wa kutoweza tena kufikia picha na kumbukumbu za miaka mingi.

Wengi wanataja athari waliopata ya afya ya akili.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment