Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Ushahidi wote kufikia sasa unaonyesha kuwa mchezaji soka wa Ureno Diogo Jota alikuwa anaendesha gari lake alipopata ajali kwenye barabara kuu ya Uhispania, na kuna uwezekano alikuwa akiendesha kwa kasi ya juu sana, polisi wanasema.
Mchezaji huyo wa Liverpool mwenye umri wa miaka 28 alifariki dunia pamoja na kaka yake André Silva, 25, wakati gari lao aina ya Lamborghini kushukiwa kupasuka tairi kaskazini-magharibi mwa mkoa wa Zamora mapema Alhamisi iliyopita.
Kikosi cha polisi nchini Uhispania kilisema wakati huo gari hilo kuna uwezekano mkubwa lilipita gari jingine katika barabara ya A52 karibu na Palacios de Sanabria lilipoacha barabara na kuwaka moto.
“Kila kitu kinaashiria uwezekano wa mwendo kasi wa juu sana kupita kiwango kinachokubalika katika [barabara kuu],” walisema polisi wa trafiki wa eneo la Zamora.
Polisi walisema wamechunguza alama zilizoachwa na tairi moja ya Lamborghini na kwamba “uchunguzi wote uliofanywa hadi sasa unaonyesha kuwa dereva wa gari lililopata ajali alikuwa Diogo Jota”.
Ripoti ya wataalam inatayarishwa kwa ajili ya mahakama juu ya ajali hiyo, na uchunguzi wao unaeleweka umefanywa kuwa mgumu zaidi na ukubwa wa moto ambao uliharibu kabisa gari.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.