Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Wanajeshi nchini Togo walitumia gesi ya kutoa machozi siku ya Alhamisi wakati mamia ya waandamanaji walipofunga barabara kuu katikati mwa jiji kutaka kiongozi wa muda mrefu Faure Gnassingbe ajiuzulu, mashahidi walizungumza na Reuters.
Gnassingbe, ambaye aliingia uongozini baada ya kifo cha baba yake, amekuwa akitawala tangu 2005 hadi Mei 2025, na kuapishwa kama rais wa Baraza la Mawaziri mwezi huo huo wa Mei, cheo chenye mamlaka makubwa na kisicho na ukomo.
Gnassingbe anakabiliwa na wito wa kujiuzulu kutoka kwa wakosoaji, juu ya mabadiliko ya katiba ya nchi ambayo yanaweza kumuweka madarakani kwa muda usiojulikana.
Asasi za kiraia na watu wenye ushawishi kwenye mitandao ya kijamii walikuwa wameitisha maandamano kuanzia Juni 26-28, baada ya serikali kusitisha kufanyika kwa maandamano mapema mwezi huu.
Familia ya Gnassingbe imetawala taifa hilo la Afrika Magharibi tangu 1967.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.