Mlanguzi wa dawa za kulevya anayesakwa zaidi nchini Ecuador akamatwa katika ‘ghala la chini ya ardhi’

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Maelezo ya picha,Adolfo Macías Villamar alipelekwa kwenye jela yenye ulinzi mkali

Polisi nchini Ecuador wamemkamata tena mtoro anayetafutwa sana nchini humo, mlanguzi wa dawa za kulevya Adolfo Macías Villamar.

Macías, pia anajulikana kwa jina la “Fito”, ni kiongozi wa Los Choneros, genge la uhalifu lenye nguvu ambalo linalaumiwa kwa mabadiliko ya Ecuador kutoka kimbilio la watalii hadi nchi yenye viwango vya juu vya mauaji katika eneo hilo.

Pia anashukiwa kuamuru kuuawa kwa mgombea urais Fernando Villavicencio mwaka 2023.

Polisi walimfuatilia hadi kwa kile walichokitaja kuwa chumba cha ghala chini ya ardhi chini ya nyumba ya kifahari katika jiji la Manta.

Msemaji wa polisi alisema hakuna risasi zilizofyatuliwa katika operesheni ya pamoja ya kumkamata ya saa 10 ya polisi na wanajeshi.

Idadi kubwa ya maafisa wa kwanza walifuatilia na kuzingira nyumba ya ghorofa tatu katika kitongoji cha Monterrey cha Manta, kwenye pwani ya Ecuador.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment