Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Tumepokea taarifa kutoka kwa Jeshi la Ulinzi la Israeli, ambalo linasema kuwa Iran imerusha makombora mengine kadhaa kuelekea Israeli.
Taarifa zinasema kuwa mifumo ya ulinzi ya Israel inafanya kazi kuzuia makombora hayo, na kwamba raia wamelazimika kukimbilia makazi ya kujilinda dhidi ya makombora.
Kikosi cha zima moto cha Israel kimesema watu watnne waliuawa katika mashambulizi kusini mwa nchi hiyo huku 22 wakijeruhiwa
Afisa wa Huduma za dharura za Israeli, Magen David Adom, alielezea tukio hilo: “Tuliona moshi mzito ukipanda kutoka eneo la athari, na tulipokaribia, tuliona uharibifu mkubwa kwa majengo kadhaa.
“Nje ya jengo moja tulimwona mwanaume akiwa amepoteza fahamu mlangoni, tulipoingia ndani kufanya upekuzi tulimkuta mwanaume na mwanamke wakiwa wamepoteza fahamu, tukaweka kituo cha kuwahudumia majeruhi na tunawafanyia uchunguzi wa kimatibabu wakazi wanaotoka nje ya majengo hayo.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.