Israel yakubali kusitisha mapigano na Iran

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Serikali ya Israel inasema imekubali pendekezo la Donald Trump la kusitisha mapigano.

Katika taarifa, Israel inasema: “itajibu kwa nguvu kwa ukiukaji wowote wa usitishaji mapigano.”

Serikali ya Israel inasema ilikubali pendekezo la kusitisha mapigano baada ya “kufikia malengo” ya mashambulizi yake dhidi ya Iran.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Israel imeondoa “Iran kama tishio mara mbili” kuanzia silaha za nyuklia hadi makombora ya balestiki.

Pia inasema Israel “imesababisha uharibifu mkubwa kwa uongozi wa kijeshi, na kuharibu maeneo kadhaa lengwa ya serikali ya Iran”.

Taarifa hiyo inaendelea kusema kwamba majeshi ya Israel, katika siku ya mwisho, “yamefikia malengo ya serikali katika kitovu cha Iran, na kuwaondoa mamia ya wanajeshi wa Basij” – ambao mara nyingi hutumika na serikali ya Iran kukandamiza waandamanaji – na “kumuua mwanasayansi mwingine mkuu wa nyuklia”.

“Israel inamshukuru Rais Trump na Marekani kwa kumuunga mkono katika ulinzi na ushiriki wao katika kuondoa tishio la nyuklia la Iran,” taarifa hiyo inaongeza.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment