Watu wanne wauawa nchini Ukraine katika shambulio jipya la Urusi

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Takriban watu wanne wameuawa katika shambulio la usiku la kombora la Urusi na ndege zisizo na rubani kwenye mji mkuu wa Ukraine Kyiv, waziri wa mambo ya ndani amesema.

Katika ujumbe kwenye mitandao ya kijamii, Ihor Klymenko amesema maeneo ya makazi, hospitali na miundombinu ya michezo iliathirika.

“Sehemu nzima ya jengo la makazi ya juu liliharibiwa” katika wilaya iliyoathirika zaidi ya Shevchenkivskyi, alisema, akiongeza kuwa baadhi ya watu wamenaswa chini ya vifusi.

Katika mkoa wa Kyiv, mwanamke mmoja aliuawa na watu wengine wawili kujeruhiwa katika shambulio la anga la Urusi, mkuu wa mkoa Mykola Kalashnyk amesema.

Hata hivyo, jeshi la Urusi halijazungumzia suala hilo.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment