Shambulio la kujitoa mhanga laua 22 kanisani Damascus – Mamlaka ya Syria

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Takriban watu 22 wameuawa na wengine 63 kujeruhiwa katika shambulio la bomu la kujitoa muhanga katika kanisa moja mjini Damascus, wizara ya afya ya Syria imesema.

Mwanamume mmoja alifyatua risasi kwa kutumia silaha katika Kanisa la Kiorthodoksi la Ugiriki la Nabii Elias katika kitongoji cha Dweila wakati wa ibada ya Jumapili jioni kabla ya kulipua vilipuzi, kulingana na wizara ya mambo ya ndani.

Ilisema mshambuliaji huyo alikuwa na uhusiano na kundi la wanajihadi la Islamic State (IS). Hakukuwa na madai ya mara moja kutoka kwa kundi lenyewe.

Picha na video kutoka ndani ya kanisa zilionyesha madhabahu iliyoharibiwa sana, viti vilivyofunikwa kwa vioo vilivyovunjika na damu iliyotapakaa kwenye kuta.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment