Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Miili ya mateka watatu wa Israel imepatikana kutoka Ukanda wa Gaza, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema.
Alithibitisha kuwa mabaki ya Yonatan Samrano, Ofra Kedar na Shai Levinson yalipatikana Jumamosi katika operesheni ya kijeshi.
“Nawashukuru makamanda wetu na wapiganaji kwa operesheni iliyofanikiwa, kwa uamuzi wao na ujasiri,” Netanyahu alisema katika taarifa yake.
Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) limefanikiwa kupata miili ya mateka wanane kutoka Gaza kufikia sasa mwezi huu.
“Operesheni ya kuwarudisha waliotekwa nyara inaendelea na inafanyika sambamba na operesheni dhidi ya Iran,” Netanyahu alisema.
“Hatutapumzika hadi tuwarudishe wote waliotekwa nyumbani – walio hai na waliokufa.”
IDF ilisema miili hiyo ilipatikana Jumamosi, lakini haikusema ni wapi katika Ukanda wa Gaza mabaki hayo yalipatikana.
Israel ilianzisha kampeni ya kijeshi huko Gaza kujibu shambulio la kuvuka mpaka lililoongozwa na Hamas tarehe 7 Oktoba 2023 ambapo takriban watu 1,200 waliuawa na wengine 251 walichukuliwa mateka.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.