Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Uingereza inatarajiwa kuweka wazi vikwazo vipya dhidi ya Urusi vilivyopangwa “kuzuia vita vya Putin” pamoja na washirika wengine wa Ukraine siku ya Jumanne.
Waziri Mkuu Sir Keir Starmer alisema hatua hizo zitaongeza shinikizo la kiuchumi kwa Ikulu ya Kremlin kumwonesha Vladimir Putin “ni kwa maslahi yake na Urusi kuonesha kwamba ana nia ya dhati kuhusu amani”.
Hata hivyo, ilionekana kutokuwa na uwezekano kwamba Marekani ingejiunga na hatua hiyo baada ya Donald Trump kuashiria upinzani wake kwa hatua zaidi wakati wa mkutano wa kilele wa G7 nchini Canada, akisema vikwazo hivyo “vinagharimu [Marekani] pesa nyingi”.
Wakati huo huo, maafisa wa Ukraine walisema watu 16 walijeruhiwa baada ya wimbi jingine la ndege zisizo na rubani na makombora kushambulia majengo katika mji wa Kyiv usiku kucha.
Katika taarifa, Sir Keir alisema yeye na washirika wengine wa G7 wanakamilisha hatua mpya katika mkutano wa Alberta, na kwamba “watapunguza mapato ya nishati ya Urusi na kupunguza pesa wanazoweza kumwaga katika vita vyao haramu”.
Mapema siku ya Jumatatu, Trump – ambaye alitangaza kuondoka katika mkutano huo mapema kutokana na mzozo unaozidi kuongezeka Mashariki ya Kati, alionesha haungi mkono mpango wa vikwazo.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.