Tunachokifahamu mpaka sasa wakati Iran na Israel zikishambuliana kwa siku ya tano

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Iran na Israel zimeendelea na mashambulizi kwa siku ya tano

Tumepokea ripoti za wimbi jipya la mashambulizi ya Wairani katika eneo la kati la Israeli wakati Tehran ikijibu mashambulizi ya Israel katika maeneo yake ya kijeshi na miundombinu mingine.

Na katika saa chache zilizopita, Rais wa Marekani Donald Trump ameondoka kwenye mkutano wa kilele wa G7 nchini Canada mapema, huku Ikulu ya Marekani ikithibitisha kuwa ana “mambo muhimu” ya kuyashughulikia huko Washington.

Aliandika kwenye mtandao wake wa kijamii muda mfupi baada ya kupanda Air Force One na kusema, licha ya maoni ya Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, hakuondoka G7 kufanya kazi ya kusitisha mapigano.

“Hakika haina uhusiano wowote” na hilo na ni “kubwa zaidi”, anasema.

Haya ndiyo mengine tunayotazama asubuhi ya leo:

  • Iran na Israel zimeshambuliana kwa siku ya tano, ingawa mashambulizi hayakuwa makali kuliko hapo awali, mwandishi wetu wa Mashariki ya Kati Hugo Bachega ameripoti.
  • Israel inasema “malengo kadhaa ya kijeshi” magharibi mwa Iran yalipigwa katika mashambulizi ya usiku kucha, ikiwa ni pamoja na makombora ya ardhini na maeneo ya kuhifadhi ndege zisizo na rubani.
  • Nchi za G7 zimetoa taarifa likihimiza “kupungua kwa uhasama” na kuitaja Iran kuwa “chanzo kikuu cha ukosefu wa utulivu na ugaidi wa kikanda”
  • Msongamano mkubwa wa magari umeonekana Tehran na foleni inaongezeka kwenye vituo vya mafuta huku wakazi wakiuhama mji mkuu.

Watu katika jiji hilo wanahoji jinsi ya kuondoka, huku mkazi mmoja akiandika mtandaoni: “Watu milioni 10 wanawezaje kuhama Tehran.?”

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment