Mzozo kati ya Iran na Israel wakatisha ushiriki wa Trump kwenye mkutano wa kilele wa G7

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alikutana na Rais wa Marekani Donald Trump katika mkutano wa G7 Jumatatu

Rais wa Marekani Donald Trump amekatiza ziara yake katika mkutano wa kilele wa G7 nchini Canada, kwani hivi karibuni atasafiri kwa ndege kurejea Washington kushughulikia mizozo inayoendelea kati ya Israel na Iran.

Milipuko inasikika mjini Tehran, muda mfupi baada ya Trump kuwaambia “kila mtu” kuondoka katika mji mkuu wa Iran mara moja.

Ving’ora nchini Israel vimesikika mara kadhaa katika saa chache zilizopita.

Trump ameliomba Baraza lake la Usalama la Kitaifa kukutana, ingawa maafisa wa Marekani wanasisitiza kuwa Marekani haishiriki katika mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment