Rais wa Zambia hatakiwi kuonekana kwenye mazishi ya mtangulizi wake, familia ya Lungu yasema

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Edgar Lungu

Rais wa zamani wa Zambia Edgar Lungu, ambaye alifariki wiki iliyopita, aliacha maagizo kwamba mrithi wake Hakainde Hichilema “hapaswi kuwa popote karibu” na mwili wake, msemaji wa familia amesema.

Haya ni matukio ya hivi punde katika mzozo mkali kuhusu mipango ya mazishi ya marehemu rais baada ya kifo chake nchini Afrika Kusini akiwa na umri wa miaka 68.

Serikali ilikuwa imepanga kusafirisha mwili wake kurejea nyumbani Jumatano, lakini ilishindwa kufanya hivyo kwa sababu ya mzozo kati ya familia ya Lungu na chama chake cha siasa, Patriotic Front (PF), kuhusu maombolezo na taratibu za mazishi.

Viongozi hao wawili walikuwa wapinzani wa muda mrefu wa kisiasa, huku Hichilema akimshinda Lungu katika uchaguzi wa 2021 baada ya kushindwa katika majaribio matano ya awali.

Katika hotuba kwa Wazambia Alhamisi jioni, rais hakurejelea moja kwa moja matakwa yaliyoripotiwa ya mtangulizi wake, lakini alikariri “wito wa amani, wito wa upendo na wito wa umoja” katika wakati huu wa “majonzi ya pamoja”.

Akionekana kuwasilisha kesi ya mazishi ya serikali, aliwataka Wazambia “kuweka kando tofauti zetu” na akatoa ombi “kuwaruhusu watu wa Zambia kumuaga rais wao wa zamani kwa heshima na inayolingana na wadhifa wa juu aliokuwa nao”.

Lungu alifariki kutokana na ugonjwa ambao haujatajwa, lakini PF ilisema wiki iliyopita kwamba alikuwa akipata “matibabu maalum” nchini Afrika Kusini.

PF ilidai kuwa Lungu alipigwa marufuku kuondoka nchini kwa miaka mingi na kwamba ikiwa angeruhusiwa kusafiri kwenda kutafuta matibabu mapema, angeweza kuwa hai mpaka sasa. Serikali imekanusha madai hayo.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment