Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Raia wa China amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kuharibu kebo ya chini ya bahari inayounganisha kisiwa kikuu cha Taiwan na visiwa vya Penghu kwenye Mlango bahari wa Taiwan.
Mtu huyo, aliyetambuliwa kwa jina lake la ukoo Wang, alikuwa nahodha wa meli iliyosajiliwa na Togo Hong Tai 58.
Uamuzi wa Mahakama ya Wilaya ya Tainan siku ya Alhamisi ni hukumu ya kwanza baada ya ripoti za miaka ya hivi karibuni za kukatwa kwa nyaya za chini ya bahari kuzunguka Taiwan.
Taipei ameishutumu Beijing kwa kuhujumu nyaya zake, na kueleza kuwa ni mbinu ya kushinikiza kisiwa kinachojitawala, ambacho China inadai kuwa eneo lake.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.