Kevin De Bruyne akubali mkataba wa miaka miwili kujiunga na Napoli

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

a

Gwiji wa Manchester City, Kevin De Bruyne, anajiandaa kuuungana na kiungo wa zamani wa Manchester united, Scott McTominay katika Ligi Kuu ya Italia (Serie A) baada ya kukubali mkataba wa miaka miwili kujiunga na mabingwa wa ligi hiyo, Napoli.

Mchezaji huyu wa kimataifa wa Ubelgiji sasa amekubali rasmi kujiunga na klabu hiyo ya Italia na anatarajiwa kusafiri kwa ajili ya vipimo vya afya na Napoli. De Bruyne atasaini mkataba wa miaka miwili, wenye kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi, kufuatia kuondoka kwake Manchester City.

De Bruyne alikuwa akivutiwa na timu kutoka Ligi Kuu ya Marekani (MLS) lakini ameamua kuendeleza maisha yake ya soka barani Ulaya na Napoli.

Kuwasili kwake kutakuwa jambo kubwa kwa klabu hiyo kufuatia ushindi wao mzuri wa taji la Serie A msimu uliopita. Ataungana na aliyekuwa kiungo wa Manchester United, Scott McTominay, katika klabu hiyo ya Italia.

McTominay alifurahia msimu mzuri wa 2024-25 na alichangia pakubwa katika mafanikio ya taji hilo la Napoli, akifunga mabao 12 ya ligi.

Katika kipindi chake akiwa Manchester City, De Bruyne ametoa pasi nyingi zaidi za mabao akiongoza ligi zote tano bora za Ulaya katika mashindano yote: pasi 170 katika mechi 422.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment