Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais wa Marekani Donald Trump alisema ameiokoa Urusi kutokana na “mambo mengi mabaya sana.”
“Vladimir Putin hatambui kwamba ikiwa sio mimi, mambo mengi mabaya yangekuwa yametokea Urusi kufikia sasa,” aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth Social, bila kutoa maelezo ya kina.
“Anacheza na moto!” – Trump aliongeza.
Siku moja kabla, baada ya siku tatu za mashambulizi makubwa ya makombora ya Urusi na ndege zisizo na rubani katika miji ya Ukraine na kuua raia 12, rais wa Marekani alimkosoa vikali Putin, ambaye Trump alisema “amekuwa mwendawazimu” kwa kuua watu “kiholela”.
Jarida la Wall Street Journal limegundua kuwa Trump anafikiria kuweka vikwazo vipya dhidi ya Urusi.
Ikulu ya Urusi ilisema Trump “anaendeshwa na hisia.”
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.