Ujerumani yamkamata aliyejitangaza ‘mfalme’ na kupiga marufuku kundi lake lenye msimamo mkali

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Aliyejitangaza “mfalme” wa Ujerumani na “watawala” wake watatu wamekamatwa na kundi lao kupigwa marufuku kwa kujaribu kupindua serikali.

Peter Fitzek, 59, alikuwa miongoni mwa wale waliokamatwa katika uvamizi wa asubuhi kwenye majimbo saba siku ya Jumanne, ambayo yalihusisha takriban maafisa 800 wa usalama.

Serikali ilipiga marufuku kikundi chao, Reichsbürger, au “raia wa Reich”, ambao wanataka kuanzisha Königreich Deutschland, au “Ufalme wa Ujerumani”.

Alexander Dobrindt, waziri wa mambo ya ndani wa Ujerumani, alilishutumu kundi hilo kwa kujaribu “kudhoofisha utawala wa sheria” kwa kuunda taifa mbadala na kueneza “simulizi ya chuki dhidi ya Wayahudi ili kuunga mkono madai yao ya mamlaka”.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment