Putin asema yuko tayari kwa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani na Ukraine

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

edx
Maelezo ya picha,Rais wa Urusi Vladimir Putin

Siku ya Jumatatu, Rais wa Urusi Vladimir Putin alipendekeza mazungumzo baina ya nchi yake na Ukraine, kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa vita.

Naye Volodymyr Zelenskiy wa Ukraine amesisitiza katika hotuba yake ya kila usiku ya video kwamba Ukraine “iko tayari kwa mazungumzo yoyote” kuhusu usitishaji mapigano ambao ungesimamisha mashambulizi kwa raia.

Viongozi hao wawili wanakabiliwa na shinikizo kutoka Marekani, ambayo imetishia kuachana na juhudi zake za kutafuta amani iwapo hakuna maendeleo yatapatikana.

Urusi na Ukraine zimesema ziko tayari kusitisha mapigano zaidi baada ya mpango wa kusitisha vita wakati Pasaka kwa saa 30 uliotangazwa na Moscow mwishoni mwa juma. Kila upande ulimtuhumu mwenzake kukiuka mpango huo.

Ukraine itashiriki katika mazungumzo na Marekani na nchi za Ulaya siku ya Jumatano mjini London, Zelenskiy alisema. Majadiliano hayo ni muendelezo wa mkutano wa Paris wiki iliyopita ambapo Marekani na mataifa ya Ulaya yalijadili njia za kumaliza vita vilivyodumu kwa zaidi ya miaka mitatu.

Putin, akizungumza na ripota wa runinga ya serikali ya Urusi, alisema mapigano yalianza tena baada ya kusita mapigano wakati wa Pasaka, na kusema Moscow, iko wazi kwa mipango yoyote ya amani na anatarajia utayari kama huo kutoka Kyiv.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment