Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Filamu zilizotengenezwa kwa usaidizi wa akili mnemba (AI) zitaweza kushinda tuzo za juu kwenye Tuzo za Oscar, kulingana na waandaaji wake.
Chuo cha Sanaa na Sayansi kilitoa sheria mpya Jumatatu ambayo ilisema matumizi ya AI na zana zingine za kidijitali “hazitasaidia wala kudhuru fursa za kupata uteuzi”.
AI ambayo inaweza kuunda maandishi, picha, sauti na video kulingana na vidokezo rahisi vya maandishi – ilisaidia kutoa baadhi ya filamu zilizotunukiwa tuzo za juu mnamo mwezi Machi.
Lakini Chuo hicho kilisema bado kitazingatia kuhusika kwa binadamu wakati wa kuchagua washindi wake.
Chuo hicho kilisema sauti yake mpya kuhusu ustahiki wa filamu zinazotengenezwa kwa kutumia zana za AI ilipendekezwa na Baraza lake la Sayansi na Teknolojia.
Chini ya mabadiliko zaidi ya sheria yaliyotangazwa Jumatatu, wanachama wa Academy lazima sasa watazame filamu zote zilizopendekezwa katika kila kitengo ili waweze kushiriki katika awamu ya mwisho ya upigaji kura, ambayo itaamua washindi.
Matumizi ya AI kwenye filamu yamekuwa mada iliyoleta gumzo baada ya Adrian Brody kutwaa tuzo ya Muigizaji Bora kwa nafasi yake katika filamu ya The Brutalist katika sherehe za mwaka huu za Oscars mnamo mwezi Machi.
Filamu hiyo ilitumia AI ili kuboresha lafudhi ya mwigizaji alipozungumza Kihungaria.
Uwezo wa teknolojia kubadilisha au kulinganisha sauti na mtindo wa msanii kwa haraka, au kufanya mabadiliko kama vile kubadilisha sura ya mtu kwa hila, umeisaidia kuwa maarufu zaidi katika utengenezaji wa muziki na filamu.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.