Marekani kufanya mazungumzo juu ya Ukraine na Ulaya

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Mjumbe maalum wa Donald Trump Steve Witkoff na mwanadiplomasia mkuu Marco Rubio watafanya mazungumzo na viongozi wa Ulaya mjini Paris leo kujadili juhudi za kumaliza vita nchini Ukraine.

Mazungumzo hayo, ambayo Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza David Lammy pia atahudhuria, ni ya kiwango cha juu zaidi cha ushirikishwaji kuhusu vita vya Ukraine tangu Februari.

Katika miezi ya hivi karibuni, serikali ya Marekani haijakuwa ikishauriana na washirika wake wa Ulaya.

Witkoff na Rubio pia, watakutana na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na timu yake.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment