Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mshambuliaji wa Manchester City Erling Haaland ametia saini mkataba mpya utakaomuwezesha kusalia katika uwanja wa Etihad hadi 2034.
Raia huyo wa Norway alijiunga na City akitokea Dortmund mwaka 2022 na amefunga mabao 111 katika mechi 126 aliyoichezea klabu hiyo tangu wakati huo.
Mkataba wa awali wa mshambuliaji huyo, ambao inasemekana ulijumuisha kipengele cha kumuwezesha kuhama, ulikuwa unamalizika mwaka 2027.
Mkataba mpya wa Haaland utamfanya mshambuliaji huyo kusalia na City hadi siku yake ya kuzaliwa ya 34 iwapo ataamua kusalia katika klabu hiyo hadi utakapokamilika katika muda wa miaka tisa na nusu.
“Nina furaha sana kusaini mkataba wangu mpya na ninatazamia kuwa kwa muda zaidi katika klabu hii kubwa,” alisema Haaland.
“Manchester City ni klabu maalum, iliyojaa wachezaji mahiri na wafuasi wa ajabu na ni mazingira ambayo humsaidia kila mtu kufikia ubora wake. “Pia namshukuru [kocha] Pep [Guardiola], wakufunzi wake, wachezaji wenzangu na kila mtu katika klabu hii kwani wote wamenisaidia sana katika miaka michache iliyopita.”
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.