Serikali za nchi za Pembe ya Afrika zimeshindwa kutetea haki za raia: HRW

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Shirka la kimataifa la kutetea haki za binadamu Human Rights Watch, limetuhumu serikali za pembe ya Afrika kwa kushindwa kulinda haki za raia wake.

Serikali ya Kenya imetuhumiwa kwa kukiuka haki za waandamanaji wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha wa mwaka wa 2024, baadhi ya waandamanaji wakiripotiwa kutekwa.
Serikali ya Kenya imetuhumiwa kwa kukiuka haki za waandamanaji wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha wa mwaka wa 2024, baadhi ya waandamanaji wakiripotiwa kutekwa. © Donwilson Odhiambo / REUTERS

Kupitia taarifa yake ya kila Mwaka Human Rights watch, limesema mataifa mengi ya Pembe na Afrika yameshindwa kuzuia raia wake dhidi ya migogoro ya kivita ambayo imekuwa ikishuhudiwa kati ya wanajeshi wa serikali na makundi ya waasi.

Human Rights Watch pia imezituhumu serikali za Afrika kwa kuwadhulumu wanaharakati na wakosowaji wa serikali.

Serikali ya Sudan Kusini pia imetuhumiwa kwa kukiuka haki za raia wake kushiriki uchaguzi baada yake kuhairisha mchakato huo.
Serikali ya Sudan Kusini pia imetuhumiwa kwa kukiuka haki za raia wake kushiriki uchaguzi baada yake kuhairisha mchakato huo. © Tony Karumba / AFP

Mkurugezi mkuu wa Human Rights Watch Tirana Hassan, amesema kwamba serikali nyingi za Afrika zimeshindwa kujizuia kupokea maoni ya wapinzani wao na hivyo baadhi kama nchini Kenya, zimekuwa zikiwakamata na hata kuwaua wakosowaji wa serikali.

Nchini Sudan kwa mujibu wa mkurugezi wa Human Rights Watch kanda ya Afrika, Mausi Segun, jeshi na wapiganaji wa RSF wamekuwa wakiwalenga raia kwa risasi na kuharibu miundo mbinu kimakusudi.

Mausi ameongeza kuwa zaidi ya watu Milioni 12 wamekimbia makazi yao nchini Sudan kutokana na vita vinavyoendelea kati ya jeshi na wapiganaji wa RSF.

Wapiganaji wa RSF nchini Sudan wametuhumiwa kwa kukiuka haki za binadamu katika vita vyao dhidi ya wanajeshi wa serikali.
Wapiganaji wa RSF nchini Sudan wametuhumiwa kwa kukiuka haki za binadamu katika vita vyao dhidi ya wanajeshi wa serikali. REUTERS – Umit Bektas

Ripoti hiyo pia imeongeza kuwa pande hasimu nchini Ethiopia na Somalia, zilizuia misaada kuwafikia waathiriwa wa vita,huku maafisa wa kutoa huduma za misaada pia wakishambuliwa na hata kuuawa.

Aidha ripoti hiyo pia imeangazia vitendo vya utekaji ambavyo vinaendelea kuripotiwa nchini Kenya, hasa baada ya mswaada wa fedha wa mwaka 2024 kukataliwa na wandaamanaji.

Mwandamanaji aliyejeruhiwa akisaidiwa wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha wa mwaka wa 2024.
Mwandamanaji aliyejeruhiwa akisaidiwa wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha wa mwaka wa 2024. © Andrew Kasuku / AP

Nchini Eritrea, Human Rights Watch imetuhumu serikali kwa kuwalazimisha raia wake kujisajili kufanya kazi kwa muda mrefu, mbali na kuwasaka raia wanakosowaji wake wanaoishi nje ya nchi na kuwakamata.

Kadhalika ripoti ya Human Right Watch imekosoa hatua ya serikali ya Sudan kusini kwa kuhairisha uchaguzi uliokuwa umeratibiwa kufanyika mwaka uliopita, hili likitajwa kuwa ukiukaji mkubwa wa raia kuwachagua viongozi wao

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment