Ukraine: Wanajeshi wa Korea Kaskazini wahimizwa kujiua ili kuepuka kukamatwa

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Korea Kaskazini inawahimiza wanajeshi wake waliotumwa Urusi kupigana dhidi ya Ukraine kujiua ili kuepusha kukamatwa, mbunge wa Korea Kusini amesema leo Jumatatu Januari 13, akinukuu idara ya ujasusi ya Seoul.

Safu ya lori za jeshi la Urusi zilizoharibiwa na makombora na vikosi vya Ukraine inaonekana kwenye barabara kuu katika wilaya ya Sudzhansky katika eneo la Kursk nchini Urusi, Agosti.
Safu ya lori za jeshi la Urusi zilizoharibiwa na makombora na vikosi vya Ukraine inaonekana kwenye barabara kuu katika wilaya ya Sudzhansky katika eneo la Kursk nchini Urusi, Agosti. AP – Anatoliy Zhdanov

“Maelezo yaliyopatikana kwa wanajeshi waliofariki yanaonyesha kwamba mamlaka ya Korea Kaskazini iliwashinikiza kujiua,” ikiwa ni pamoja na “kujilipua (…) kabla ya kukamatwa,” Lee Seong-kweun amewaambia waandishi wa habari, akinukuu taarifa kutoka kwa idara ya ujasusi ya Korea Kusini.

“Makadirio yanaonyesha kuwa idadi ya waliopoteza maisha kati ya vikosi vya Korea Kaskazini imezidi 3,000, ikiwa ni pamoja na takriban 300 waliofariki na 2,700 kujeruhiwa,” Lee Seong-kweun amewaambia waandishi wa habari baada ya taarifa ya kijasusi ya Korea Kusini, shirika la habari la AFP limeripoti.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment