Kipenga cha Michezo-13-01-2025-RFA

Tetesi za soka Ulaya Jumatatu: AC Milan, Inter Milan wamuwania Walker

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

 Kyle Walker

Mlinzi wa kulia wa Uingereza Kyle Walker, 34, anatazamiwa kusaini kandarasi ya miaka miwili na nusu na AC Milan na kufanikiwa kuhama kutoka Manchester City siku zijazo. (Telegraph)

Walker anaweza kujiunga na wapinzani wa Milan Inter Milan kwa mkopo wa msimu mzima. (Mail)

Timu kutoka Saudi Pro League zimesalia na nia ya kumsajili Walker, lakini beki huyo anataka kusalia Ulaya. (Sky Sports)

Meneja wa Napoli Antonio Conte anamtaka winga wa Manchester United Alejandro Garnacho, 20, kuchukua nafasi ya winga wa Georgia Khvicha Kvaratskhelia, 23, ambaye anatarajiwa kuhamia Paris St-Germain. (Sport Italia)

Beki wa Uruguay Ronald Araujo, ambaye amekuwa akihusishwa na Juventus, anataka kuondoka Barcelona haraka iwezekanavyo, lakini klabu hiyo ya Catalan ina nia ya kumbakisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Mundo Deportivo)

Beki wa Ujerumani Mats Hummels, 36, hana haraka ya kuanza mazungumzo juu ya kuongezwa kwa mkataba katika klabu ya Roma, huku mkataba wake wa sasa ukitarajiwa kukamilika mwezi Juni. (Soka Italia)

West Ham wako tayari kuleta mshambuliaji mpya baada ya kujua ukubwa wa jeraha la msuli wa mshambuliaji wa Ujerumani Niclas Fullkrug, 31, alilopata katika mechi ya Ijumaa ya Kombe la FA dhidi ya Aston Villa. (Fabrizio Romano)

Niclas Fullkrug

Monaco wamewasilisha ombi la kumnunua kiungo wa West Ham Edson Alvarez, 27, baada ya ofa ya kumchukua kwa mkopo mchezaji huyo wa kimataifa wa Mexico kukataliwa na The Hammers. (Fabrizio Romano)

Mshambuliaji wa Brighton ya Jamhuri ya Ireland Evan Ferguson, 20, na mshambuliaji wa Manchester United Muingereza Marcus Rashford, 27, wamehusishwa na uhamisho wa mkopo kwenda West Ham. (TBR Football)

Marcus Rashford

Atalanta wanataka kukamilisha usajili wa Januari wa mshambuliaji wa Everton na England Dominic Calvert-Lewin, 27, ambaye amekuwa akihusishwa na uhamisho wa kuelekea Newcastle United msimu wa joto kwa uhamisho wa bure. (Sun)

Bayern Munich wamempa mlinzi wa Canada Alphonso Davies, 24, mkataba mpya wenye thamani ya euro 25m (£21m) huku Real Madrid wakipania kumsajili kwa uhamisho wa bila malipo msimu wa joto. (Marca)

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment