Vifo vya watu 10 vyathibitishwa katika moto mkali huko Los Angeles

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

edc

Moto wa nyika huko Los Angeles umesababisha vifo vya takribani watu 10, huku maafisa wakionya kwamba upepo mkali unaweza kuzidisha moto huo.

Mkuu zima moto katika eneo hilo ameiambia BBC kwa sasa hakuna “ushahidi wa uhakika” kwamba moto huo ulianzishwa kimakusudi.

Naye mkuu wa Polisi wa Kaunti ya Los Angeles, Robert Luna anasema si salama kufikia maeneo mengi yaliyoathiriwa, huku akitarajia idadi ya vifo kuongezeka.

Takriban nyumba na majengo ya kibiashara 100,000 hayana umeme huko Los Angeles, kulingana na tovuti inayofuatilia kukatika kwa umeme nchini Marekani, huku zaidi ya watu 100,000 wamehamishwa katika eneo la Los Angeles

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment